Nafasi za Kazi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais - Pemba

Maelezo

Chanzo: Utumishi Zanzibar



Tarehe Iliyotolewa: 2020-08-31



Kituo cha Kazi/Tukio: Zanzibar
Imetembelewa mara! 21786 ... Deadline: 2020-09-04 12:30:00

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi kwa ajili ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais - Pemba kama ifuatavyo:-


1. Afisa Uhusiano Daraja la II “Nafasi 1” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Uhusiano kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.



2. Afisa Kumbukumbu Msaidizi Daraja la III “Nafasi 1” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Stashahada katika fani ya Utunzaji Kumbukumbu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar




3. Fundi Umeme Daraja la II “Nafasi 1” - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Ufundi wa Umeme kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.



4. Fundi Vipaza Sauti Daraja la II “Nafasi 1” - Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Ufundi wa Umeme au Mawasiliano ya Umma au Ufundi Vipaza Sauti kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.


5. Dobi Daraja la III “Nafasi 2” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu elimu ya Sekondari na kupata cheti cha Uhudumu au Udobi au Utunzaji Nyumba kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.


6. Watunza Bustani Daraja la III “Nafasi 3” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amemaliza elimu ya Sekondari.



7. Wahudumu Daraja la III “Nafasi 2” – Pemba
Sifa za Waombaji:
• Awe ni Mzanzibari.
• Awe amehitimu Stashahada au Cheti katika fani ya Uhudumu kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.



Jinsi ya Kuomba:
•Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:-




KATIBU,
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI,
S. L. P 1587 - ZANZIBAR.

• Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Jumba la Wananchi Forodhani Zanzibar wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Chake Chake Pemba.

Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:-

a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari)
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa.
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari.
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni.
f) N.B: Atakaewasilisha ‘Statement of Result’ au ‘Progressive Report’ maombi yake hayatazingatiwa.
g) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 04 Septemba, 2020 wakati wa saa za kazi
 



Share via Whatsapp
Advertise with us

©2024 Zenji Shoppazz . Haki zote zimehifadhiwa | Imetengenezwa na W3layouts and Zenji Shoppazz Chagua lugha : English